Saturday, August 28, 2010

Ravalomanana apewa hukumu ya kazi ngumu


ANTANANARIVO
Rais wa zamani wa Madagascar   Marc Ravalomanana  jana alihukumiwa kutumikia  kifungo cha  maisha   jela  na   kazi ngumu , kuhusiana na mauaji yaliyofanyika Februari mwaka wa 2009. Hii ni hukumu ya tatu dhidi ya Ravalomanana tangu aondolewe madarakani. Wakili wa Ravalomanana alisema rais huyo ambaye anaishi uhamishoni Afrika Kusini, alihukumiwa  kwa  kuhusika  na mauaji na kuwa mshiriki katika mauaji. Februari mwaka 2009 walinzi wa rais Ravalomanana waliwafyatulia risasi wafuasi wa Andry Rajoelina, rais wa sasa wa kisiwa hicho na kuwaua watu 30 na kuwajeruhi wengine 100. Akiwa nchini Afrika Kusini, Ravalomanana aliikejeli  hukumu hiyo akiitaja kama ya kipuuzi.

No comments:

Post a Comment